VIKUNDI KATIKA KANISA - PHM TANZANIA - SEHEMU YA IZIWA

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, September 26, 2017

VIKUNDI KATIKA KANISA


Jumuiya ya Watetezi wa Imani - Community of Faith Defenders (CFDs) ni moja ya Idara ndani ya kanisa la Pentecostal Holiness Mission (PHM) yenye malengo chanya kwa kanisa kama Idara zingine. Hii ni idara ambayo inayohusisha vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 50. Idara ya CFDs katika utendaji wa kazi imegawanyika katika ngazi nne, kuanzia ngazi ya chini yaani kanisa la mahali hadi ngazi ya juu ya kitaifa kama ifuatavyo:- CFDs katika kanisa la mahali, Sehemu (Section), Jimbo na Taifa.

Idara ya CFDs kwa kipindi cha miaka kumi (10) kuanzia mwaka 2017 hadi 2027 imekuwa na malengo makuu kadha ya kimkakati. Katika utekelezaji wake wa majukumu hayo ya kimkakati, CFDs unahusisha uongozi wa Taifa, Majimbo, Sehemu, Makanisa ya mahali na wana CFDs wote kwa ujumula nchini. Ili kulifanikisha zoezi zima hili tumesimamia kauli mbiu yetu inayosema “Mabadiliko ya kiroho na kiuchumi katika PHM na CFDs inawezekana!! Wajibika!!” Lengo likiwa ni kuwajibika ipasavyo kwa kila mwana Idara kupitia uongozi uliopo ili kuleta maendeleo yenye tija ndani ya Idara. Hii ni kulingana na vipaumbele maalumu vya utekelezaji vya kimkakati vilivyowekwa kwa miaka hiyo. Hali hii inalenga ukuaji wa kanisa kiroho na kiuchumi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi zaidi.
====================================================================



PENTECOSTAL HOLINESS MISSION
COMMUNITY OF FAITH DEFENDERS (CFDs)
(JUMUIYA YA WATETEZI WA IMANI)
HEADQUATERS

OFFICE CORNER                                                                                              
MOROGORO/MABIBO ROAD
P.O.BOX. 22503
DAR ES SALAAM
TANZANIA


TEL     +255 222 401225
MOB:  +255 765 413238                                                                                         
EMAIL phmcfdstaifa@yahoo.com            or
              phmacfdstaifa@gmail.com


No comments:

Post a Comment

test banner

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here